KWANINI NI VIGUMU KURUDISHA IMANI KWA MTU ALIYEKUSALITI?
" kuna kipindi huwa nailaumu nafsi yangu nikisema si yalikwisha na nilikwisha msamehe mbona simwamini tena?"
anasema Monica
si monica peke yake anaelalamikia jambo hili maelfu ya watu ulimwenguni kote wameshindwa kabisa kuwaamini tena wenzi wao walio wasaliti.
" kila anaponiambia naomba uniamini mpenzi mimi si yule wa mwanzo ni kama ananiambia kwamba sasa ndiyo naenda kukusaliti kwa kweli siwezi tena kumwamini"
anasema Abdalla.
huenda hata wewe ukajikuta katika hali ya namna hiyo hiyo ukikubwa na tatizo kama hili.
una fikiri ipo namna kurejesha imani yako tena?
' imani ni kitu kigumu zaidi kukirejesha na kinaitaji muda kukifanikisha. '
hivyo hupaswi kuilaumu nafsi yako , kuirudisha imani yako kunategemea sana vitendo vya mwenzi wako aliyekusaliti pamoja na kusamehe na kusahau yale aliyoyatenda.
kama yeye hatokuwa na bidii za kukushawishi wewe umwamini tena itakuwia vigumu sana wewe kurudisha imani kwake.
kama hatoonyesha ushirikiano wowote au pengine akaendeleza vitendo vyake vya usaliti kamwe huwezi kurudisha imani kwake
hata kama unampenda kiasi gani.
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home